Header Ads

LightBlog

Barabara ya Dar es Salaam iliyoleta ugomvi



Jana tarehe 8/8/217 niliokoa vijana wawili wasitoane macho na kung’oana meno. Nilikuta wamekabana koo. Nikaamuru dereva wangu asimame.

Wakati ninatoka katika gari, wakawa ndio wanaangushana chini na kuanza kuviringishana kwenye vumbi huku wakipigana ngumi kichwani.

Ilichukua kama dakika tano hivi kuwaachanisha. Nikauliza kilichowasibu.

Mmoja akasema: “…huyu ni mpumbavu. Anasema kuwa barabara hii ilikuwa ya lami lakini sasa ni udongo mtupu. Mimi nikamwambia haiwezekani lami itoke kiasi cha kubaki vumbi namna hii; lakini yeye anabisha. Ndipo tukashikana…”

Mwingine akasema: “…hili jinga tu. Mimi nimekuwa nikipita barabara hii kwa miaka mitano sasa nikienda shule. Ilikuwa ya udongo; baadaye wakaweka lami. Sasa lami imekwisha yote katika kipindi cha miaka mitatu hivi na imerudia hali ileile ya vumbi.

“Huyu (aliyekuwa akipigana naye) hakuwepo hapa lakini anabisha na kuanza kunitukana na kusema kuwa lami haiwezi kuisha katika kipindi hicho. Ndio umekuta tumekamatana lakini ni kutokana na huyu kunitukana.”

“Barabara ya Ugomvi” ni ile inayochomoka kwenye Barabara ya Shekilango, Sinza Afrika Sana kupitia Kituo cha Polisi cha Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Ni kweli, barabara hii ilikuwa vumbi wakati wa jua na matope wakati wa mvua. Wakaweka kifusi (sijui nani!). Baadaye wakaweka lami (sijui nani) ikateleza na karibu dunia yote ikahamia huko. Leo ni vumbi tupu.


Je, unaweza kusaidia kuoroshesha visababishi vya ugomvi huu wa kung’oana meno na macho? Barabara yenyewe ni hii katika picha.

No comments

Powered by Blogger.