Header Ads

LightBlog

Spika Makinda anafanya kazi ya nani?


Fastafasta ya serikali

Hii kazi ambayo Spika Anne Makinda anafanya; ni kazi ya shetani. Hakuna jina wala njia nyingine yoyote ya kuiita. Huku kutoa nje ya vikao (Ijumaa na Jumamosi), wabunge wanaopinga miswada ya kinyonyaji - ambayo ni wazi kabisa kwamba imebeba maslahi ya wanyakazi na siyo wananchi - iwe kwa msuko wa makusudi au bila kujua; ni kufanya "kazi chafu."

Hapa hakuna swala la vyama na itikadi za vyama. Hapa kuna maslahi ya nchi. Na Makinda, akiwa kiongozi wa Bunge, alipaswa kuelewa hili; kwamba miswada ya gesi, petroli na uwazi, siyo ya kupitisha bungeni kama mifugo inavyopitishwa kwenye josho. Inahitaji fikra pevu na muda wa kutosha. Basi kwa tendo lake, Makinda atakuwa anajua kilicho nyuma ya pazia; nyuma ya fastafasta - na hii yaweza kuwa ni kulinda mafao ya binafsi na siyo taifa na watu wake.

Kinachosikitisha zaidi ni kwamba wabunge wengi wa CCM, baada ya kuona wenzao wa upinzani wametolewa nje, wakaacha kujadili miswada hiyo; wakaanza kujadili na kulaani wabunge waliotolewa nje; wakaanza kupendekeza hatua kali zaidi dhidi ya waliotolewa nje; na wakaanza kuimba ngonjera za wasifu kwa spika aliyekosa ujasiri; akakosa ukomavu; akakosa maarifa na hekima. Shida!

Click here to go to my facebook page. 

No comments

Powered by Blogger.