Header Ads

LightBlog

Hawakuandikishwa: wameachwa au wamekataa?

Kila mwananchi ana haki ya kujiadikisha ili aweze 
kushiriki uchaguzi katika eneo lake - Oktoba 2015. 


WOTE AMBAO HAWAKUANDIKISHWA  
KATIKA DAFTARI LA WAPIGAKURA
 WAWEZA KUJITOKEZA KUPITIA HAPA

Kwenye mawasiliano ya imeili mjadala unaendelea. Waandishi wa habari na wasio waandishi wanakusanya majina ya watu ambao hawakuandikishwa katika daftari la kupiga kura - kwa sababu zozote zile - katika maeneo ambako tayari Tume ya Uchaguzi imetangaza kuwa imekamilisha uandikishaji. TUWAFAHAMU WAO NA IDADI YAO. NAO WAFAHAMIANE.

Je, wewe unajua nani hakuandikishwa au anadai kutoandikishwa katika eneo lako? Tupe taarifa kwa mtindo huu hapa:

Unachoombwa kufanya:
1. Sikiliza.
2. Pata anayedai kuwa hakuandikishwa.
3. Pata majina yake matatu.
4. Pata anakoishi na anwani yake/simu yake.
5. Pata kitambulisho chake chochote – kama kipo.
6. Pata maelezo: Kwanini hakuandikishwa/mazingira.
7. Rekodi/nukuu kauli anazodai kuambiwa na waandikishaji.
8. Kama simu yako ina kamera, pata picha yake.
9. Peleka taarifa zako kwa:

       ndimara2014@gmail.com
10. Kwa maulizo zaidi ita: 0713 61 48 72.



Maelekezo yaliyopelekwa kwa waandishi wa habari na wadau wa habari sehemu mbalimbali nchini ni kama ifuatavyo:

Kuwa Jicho, Sikio na Mdomo wa Jamii


OKTOBA mwaka huu (2015) kutakuwa na Uchaguzi Mkuu – kuchagua madiwani, wabunge na rais. Hivi sasa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) inafanya kazi ya kuandikisha wapigakura.


Tayari Tume imetangaza kumaliza kazi ya kuandikisha wapigakura katika baadhi ya wilaya; LAKINI tangazo hilo linafuatiwa mgongoni na sauti nyingi za wananchi wanaodai kuwa hawakuandikishwa.

Nani hakuandikishwa? Yuko wapi? Ana maelezo yapi kuhusu kutoandikishwa?

Katika eneo unamoishi au uliko sasa kikazi au kwa matembezi, kuna wananchi wanaodai kuwa Tume haikuwaandikisha. Wangependa kuandikishwa ili washiriki kuchagua viongozi wanaoona watawatumikia; au watakaowawajibisha pale watakaposhindwa kuwahudumia.

Moja ya kazi kuu za mwandishi wa habari ni kupaza sauti za wananchi; ili wanachofikiri, wanachotaka, wanachosema na wanachotenda au kutendewa, kiweze kusikika kwa wengine, wakiwemo wenye mamlaka na dola kwa jumla.

Ukiwa jicho la nyongeza la jamii; sikio la nyongeza la jamii; na mdomo wa nyongeza wa jamii; sasa tafuta na kurekodi, kwa manufaa ya umma na watawala; watu wote katika eneo ulipo au unakokwenda, ambao kilio chao ni kutoadikishwa.

Siyo rahisi kuorodhesha kila mmoja ambaye anadai kutoandikishwa; lakini una uwezo wa kufikia hadi watu 50 au zaidi ili kuweka ushahidi unaoweza kusaidia kuleta utatuzi na hata mabadiliko makubwa katika jamii. Ni heshima iliyoje kuwa mmoja wa vibarua wa umma na kutambuliwa hivyo!

Tuko waandishi saba. Tunakushirikisha wewe na mwishoni mwa kazi hii ya kujituma kukutana na wenyekilio na kukusanya taarifa hizi, utakuwa tayari sehemu ya kundi hili. 

Haya ni mazingira yaliyosheheni FURSA za kuinua na kuibua vipaji vya waandishi wa habari. Ni fursa za kutumikia umma kwa njia ya kurekodi ukweli, tena kuurekodi kwa usahihi; ili wahusika waweze kuchukua hatua. Ni fursa zinazozaa, kulea na kukomaza umahiri katika taaluma ya habari. 

Unachoombwa kufanya:

1.     Sikiliza.
2.     Pata anayedai kuwa hakuandikishwa.
3.     Pata majina yake matatu.
4.     Pata anakoishi na anwani yake/simu yake.
5.     Pata kitambulisho chake chochote – kama kipo.
6.     Pata maelezo: Kwanini hakuandikishwa/mazingira.
7.     Rekodi kauli anazodai kuambiwa na waandikishaji.
8.     Kama simu yako ina kamera, pata picha yake.
Peleka taarifa zako kwa ndimara2014@gmail.com
10.                        Kwa maulizo ita: 0713 61 48 72.
Asanteni,

Ndimara Tegambwage
 





No comments

Powered by Blogger.